RAIS MWINYI AFUTURISHA WANANCHI WA MKOA WA MJINI MAGHARIBI

 





Na mwandishi wetu

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt, Hussein Ali Mwinyi amejumuika na Wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi katika  kula futari ya pamoja aliyowaandalia.

Hafla hiyo imefanyika Ukumbi wa Idrissa Abdulwakil Kikwajuni ,Wilaya ya Mjini , Mkoa wa Mjini  Magharibi.

Akizungumza katika Futari Hiyo  Rais Dkt, Mwinyi  amewahimiza Waumini wa Dini ya Kiislamu na Wananchi Kuendelea kuiombea Nchi Amani pamoja na Viongozi Wakuu Ili waendelee kuiongoza Nchi kwa Amani na  waendelee kutekeleza Mambo ya Maendeleo.

Hafla hiyo pia imehudhuriwa  na Mke wa  Rais wa Zanzibar,Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation  Mama  Mariam Mwinyi.

Rais Dkt, Mwinyi amekuwa na Utaratibu huo kila Mwaka  unaofanyika  katika Mikoa yote ya Zanzibar .














Post a Comment

0 Comments