TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA 47 WA MILIKI UBUNIFU

 


Na Mwandishi Wetu

Tanzania inashiriki katika mkutano wa 47 wa Shirika la Miliki Ubunifu Afrika (ARIPO) unaojadili taarifa  ya mwaka  pamoja na kupitisha mpango kazi wa mwaka 2024.
 
Washiriki wa mkutano huo wa siku nne unaofanyika Gaborone Botswana  ni Wakuu wa Ofisi za Miliki Ubunifu kutoka nchi wanachama wa ARIPO, ambapo kwa upande wa Tanzania Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA Bw. Godfrey Nyaisa ameongoza Msafara wa Tanzania kwa kuambatana na Maafisa wa BRELA Bw. Seka Kasera na Bw. Alex Mashamba huku upande wa Zanzibar ukiwakilishwa na Bw.  Mustafa Haji kutoka Wakala Usajili wa  Biashara na Mali Zanzibar (BPRA).
 
Mkutano huo wa siku nne unaohudhuriwa na nchi wanachama 22 za Afrika umefunguliwa rasmi leo tarehe 20 Novemba, 2023 na Waziri wa Viwanda na Biashara wa Botswana Mhe. Mmusi Kgafela na utafuatiwa na Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa nchi wanachama wa ARIPO.
 
Katika  mkutano huo ARIPO itawasilisha taarifa ya utendaji kazi ya mwaka kwa wanachama  ambayo itajadiliwa na Wanachama na kuipitisha kisha kuwasilisha mpango kazi  kwa mwaka 2024.

Post a Comment

0 Comments