Taarifa kwa Umma
KIONGOZI wa chama cha ACT Wazalendo, ndugu Zitto Kabwe,anatarajia kufanya ziara katika majimbo 8 ya Mkoa wa Kigoma kuanzia Novemba 14 mpaka Disemba 2, 2023.
Katika ziara hiyo ndugu Zitto atakutana na Viongozi wa matawi 482 (Vijiji 306 na Mitaa 176), Kata 156 ya Majimbo yote 8,Kwa ajili ya kujadiliana na Viongozi wa ngazi zote za ACT Wazalendo kuhusu maandalizi na utayari wa chama kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024.
Pia ndugu Zitto atazungumza na wananchi kupitia mikutano ya hadhara katika Majimbo yote ya Mkoa wa Kigoma.
Abdallah Khamis
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano,Ofisi ya Wasemaji wa Kisekta ACT Wazalendo
Dar es salaam
Novemba 11, 2023
0 Comments