MKUU WA WILAYA YA MBINGA ATEMBELEA ENEO LA UJENZI WA MRADI WA SHULE YA MPYA YA KISASA YA SEKONDARI, KATA YA LITEMBO

 


Na mwandishi wetu


Mkuu wa Wilaya Mbinga Mhe. Kisare Makori leo tarehe 6-9-2024 ametembelea eneo la ujenzi wa mradi wa  shule ya sekondari mpya ya kisasa ya kata ya Litembo. Lengo la ziara hiyo ni  kukagua maendeleo ya utekelezaji wa  mradi huo  wa ujenzi wa shule mpya katika kata hiyo.


Mradi huo unatekelezwa kwa gharama ya shilingi  milioni 560 ambazo zimetolewa na serikali kuu ikiwa ni muendelezo wa mpango wa serikali ya awamu ya sita  kuhakikisha kata zote za wilaya ya Mbinga zinakuwa na shule za sekondari. 

 Mradi huo kwa sasa upo katika hatua ya msingi ya utekelezaji wake.


Akizungumuza na baadhi ya  wananchi wa kata ya Litembo waliojitokeza katika eneo la mradi huo kwa ajili ya kujitolea kuchimba msingi , Mkuu wa Wilaya amemushukuru sana  Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia wilaya ya Mbinga jumla ya shilingi bilioni 1.1 kwa ajili ya ujenzi wa shule mbili mpya za sekondari katika kata ya Litembo na Nyoni.

Aliendelea kusema kwamba ni ukweli usiopingika kwamba tunaye Rais ambaye amejitolea kidete katika kuhakikisha anasogeza na  kufikisha huduma mbalimbali za kijamii kwa wananchi wake kama ambavyo alihaidi na sisi Mbinga ni mashahidi tumeletewa sh milioni 560 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya kisasa ya Litembo na shilingi milioni 560 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya  sekondari ya  Nyoni.


Aidha Mkuu wa Wilaya  amewapongeza viongozi na wananchi wa kata ya Litembo kwa kushiriki kikamilifu na kujitokeza kuchangia nguvu zao katika utekelezaji wa mradi huo. 


Mkuu wa Wilaya pia  ametoa rai kwa viongozi wote wanaosimamia mradi huo kuhakikisha kwamba mradi unakamilika kwa wakati kama ambavyo imekwishaelekezwa na serikali  na kuzingatia ubora na viwango katika utekelezaji wake.





Post a Comment

0 Comments