CCM:Uchaguzi si jambo la ghafla tumejiandaa kushinda 2025

 



Na Mwandishi  Wetu, Zanzibar 


Chama Cha Mapinduzi  kimewataka wana CCM kutambua uchaguzi mkuu  si jambo la dharura na ghafla  hivyo kila MwanaCCM  ajue  wakati  umefika wa  kusimama pamoja  kutafuta ushindi wa chama. 

Pia chama hicho  kimewahimiza wanachama  wake wote , kujitokeza  itakapoanza ngwe za  kampeni na siku  ya upigaji kura  kwani uchaguzi ni suala la kufa na kupona.

Katibu wa Kamati Maalum  ya NEC  Zanzibar  Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Khamis Mbeto Khamis ametoa maelezo hayo huku akiwataka wanachama wote kushiriki kwa nguvu  zote  kuwachagua wagombea toka  CCM. 

Mbeto  alisema   ni muhimu kwa kila mwanachama wa CCM ajue  kuwa kujitokeza kwao  siku ya  kupiga  kura ,wajione wamebeba urithi wa  wazazi  unaotokana na vyama vya  TANU na ASP vilivyoleta Uhuru na Mapinduzi. 

Alisema Uchaguzi ndio unaoviweka Vyama vya Siasa madarakani  hivyo  anawahimiza wananchi wa  Tanzania na Zanzibar ,  kwenda kuwapigia kura wagombea Urais  wa CCM,  Dk Samia  Suluhu  Hassan na Dk Hussein Ali  Mwinyi .

"Uchaguzi  si jambo  na zoezi la  ghafla. Kila baada ya miaka mitano hufanyika. Pamoja na CCM  kuionyesha dunia nchi zetu zinaongozwa kidemokrasia . Matumaini yote ya wananchi yamebebwa na sera  CCM si vinginevyo" Alisema Mbeto 

Aidha, Katibu  huyo Mwenezi  alisema kipimo  cha kuchaguliwa tena Marais Dk Samia na Dk Mwinyi kinatokana na ufanisi wa  kazi kubwa walizozifanya  miaka mitano iliopita. 

'CCM kinashiriki Uchaguzi  mkuu wa Mwaka 2025/2030 kikiwa na matumaini  makubwa  ya kushinda kuliko  miaka yote  . Kitashinda baada ya kimtetimiiza wajibu na ahadi  zake kwa jamii na kwa  maendeleo ya  nchi "Alisema Mbeto 

Pia alisema  kutokana na kufanyika kazi kubwa iliotokana na  utendaji wenye  ufanisi na utekelezaji wa kisera,  CCM kitashiriki  uchaguzi  huo oktoba   kwa lengo moja tu la  kushinda na kuongoza dola. 

"Tumetekeleza ahadi zetu  zote kama chama tawala . Marais wetu wametoka jasho na kutimiza wajibu kwa  vitendo na utumishi uliotukuka. Kazi iliobaki ipo kwa wananchi wanaosubiri kutia tiki katika karatasi za kura" Aliileza

Hata hivyo Katibu  huyo  Mwenezi  alisema Chama Cha Mapimduzi lazima kishinde kwakuwa kinaaminiwa  na Wananchi waliio wengi  ,kina viongozi  Wazalendo, sera makini na Siasa  safi .

"Chama chetu hakisubiri kudandia au kuvizia  wagombea wanaotemwa na vyama vingine ili  wagomba urais na ubunge  . Tuna mamia ya  wagombea madhubuti  wanaoeleweka na Wazalendo wasiotiliwa shaka yoyote "Alisiaitiza Mbeto

Post a Comment

0 Comments