Na mwandishi wetu
Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi, amewasili na kupokewa na Viongozi wa CCM wa Mkoa wa Kusini Pemba kichama, tayari kwa mazungumzo na Wajumbe wa Kamati za Siasa za Halmashauri kuu ya CCM ngazi ya Tawi, Wadi, Majimbo, Wilaya na Mkoa.
Katika viwanja vya Tibirinzi Mkoa wa Kusini Pemba Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndugu Mohamed Said Dimwa amewaongoza viongozi wa CCM kumlaki Dk. Mwinyi alipowasili.
📅 22 Agosti 2024
0 Comments