CHAMA CHA NLD YAMLAMBA MWENYEKITI WA BODI YA WADHIMINI KUTOKA CHAMA CHA ADC

 





Na mwandishi wetu

Makamu Mwenyekiti wa bodi ya wadhamini wa Chama cha ADC, Mhe. Twaha Mngatwa, akikabidhiwa kadi ya Chama cha NLD na Katibu Mkuu wa chama hicho, Mhe. Doyo Hassan Doyo. Hii inakuja baada ya Chama cha NLD mwezi uliyopita Jijini Dar es Salaam kupokea wanachama 200 kutoka ADC, na sasa chama hicho kimepokea zaidi ya wanachama 100 kutoka Handeni.

Hatua hii inaonyesha kuimarika kwa chama hicho, huku NLD ikiongeza nguvu ya kisiasa na ushawishi katika maeneo mbalimbali nchini, hasa katika kipindi hichi cha uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji


*By Ombe B. Kilonzo*

Post a Comment

0 Comments