TAMASHA LA UTAMADUNI WA MNYAKYUSA LA LINDIMA DAR

 






Na mwandishi wetu

TAMASHA la Utamaduni wa Mtanzania, Siku ya Jamii ya Wanyakyusa  katika Kijiji cha Makumbusho ya Taifa,Kijitonyama, jijini Dar es  Salaam,  limegusa hisia za wadau wengi  hapa nchini ambao wametaka liwe endelevu.

Tamasha hilo lilianza jana, limefunguliwa na  Mwenyekiti wa Chama Chapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya,  Patrick Mwalunenge,ambaye amesema litakuwa chachu  ya kuiunganisha jamii ya wanyakyusa na kuunda chombo  kitakacho simamia jamii hiyo.

“Nitasimamiaa kuunda chombo maalumu cha kutambua na kusimamia juhudi  za jamii ya  wanyakyusa. Tutashirikiana  na Makumbusho ya Taifa na wadau mbalimbali kuona namna bora ya kufanya  kuunda chombo hiki,”amesema Mwalunenge.

Mwalunenge,a,ameeleza  chombo hicho kitakuwa na majumu mbalimbali  yakiwemo ya  kujadili changamoto na mafanikio ya wanyakyusa, hususan masuala ya elimu, fursa za maendeleo na maadili ya utamaduni.

Awali Chifu wa Wanyakyusa, Uswege Mwakabulufu, alisema tamasha hilo limetoa ujumbe mzito kwa jamii hiyo kuenzi utamaduni wake,  huku akiwataka wana jamii  kujikita katika kusomesha  watoto na kufanya kazi kujiletea kipato.

Mwenyekiti wa Kamati ya Mandalizi ya Tamasha hilo,  Enelen Mwakapila,alisema, limehusisha, matukio mbalimbali, ikiwemo uzinduzi wa nyumba za asili za wanyakyusa katika Kijiji cha Makumbusho ya Taifa, Kijitonyama, jijini Dar es Salaam, chakula, mavazi, burudani za ngoma za asili ,  vinyaji na mavazi.

Katika  tamasha hilo linalohitimishwa kesho, ngoma za asili  za  kinyakyusa za  ing’oma  ambazo ni Lugombo ya Wilaya ya Kyela na  Kisiba ya Rungwe, zimekuwa kivutio kikubwa huku bendi ya muziki wa dansi ya Town  Band ikiburudisha.

Post a Comment

0 Comments