Mbeto ampa onyo kali Jussa akimtaka apambane na chama chake

 



Na Mwandishi  Wetu, Zanzibar 


Chama Cha Mapinduzi kimemtaka Makamu Mwenyekiti  wa ACT Wazalendo, Ismail  Jussa Ladhu,kuelewa kuwa siku zote   mambo ya ngoswe huachiwa ngoswe wenyewe kwani yanayoendelea ndani ya CCM yanawahusu wana CCM  wenyewe.

Pia chama hicho  kimemueleza Jussa atautambua ukweli wa mambo na  kukubalika kwa Rais Dk Hussein Ali  Mwinyi  ifikapo  Oktoba Mwaka huu. 

Hayo yametamkwa na  Katibu  wa Kamati  Maalum  ya NEC  Zanzibar, Idara  ya Itikadi , Uenezi na Mafunzo , Khamis Mbeto Khamis aliyesema matokeo ya Uchaguzi  Mkuu  ndio yatakayokata ngebe na kidomodomo cha  Jussa.

Mbeto alisema kwa miaka yote tokea mwaka 1995 hadi 2020,  CUF   baadae ACT , vilikuwa vikimsimamisha mgombea mmoja  wa urais Hayati Maalim  Seif Sharif Hamad na CCM hakikuwahi kuhoji. 

Alisema CCM  hakikusema lolote  au kuingilia matakwa ya demokrasia na maamuzi ya chama hicho wala kuhoji kwanini mgombea anakuwa  mtu huyo  huyo miaka kwa miaka.

"Ni ajabu kumsikia Ian Smithi wa  Zanzibar  akiingilia mambo ya CCM na kutaka Dk Mwinyi  asiwe mgombea Urais Zanzibar . Tunaijua  hofu alonayo Jussa na wenzake ni bidii,utayari  na uchapakazi wa Rais Dk Mwinyi  "Alisema Mbeto 

Aidha, Katibu huyo  Mwenezi  alisema kama kweli Jussa  ni Mwanademokrasia wa kweli  ilikuwaje miongo yote  hiyo ndani chama chao wawe na mgombea  mmoja wa kudumu .

"Jussa  anza kutoa boriti kwenye jicho lako kabla hujakitoa kibanzi kwenye  jicho la mwenzako. Maalim  Seif  amekuwa akigombea Urais kila mwaka hakuwahi kumkosoa .Mambo ya CCM hutawezi  waachie  waamue wana CCM  wenyewe "Alisema Mbeto 

Pia  Katibu  huyo Mwenezi  amekitaka  ACT kutoidanganye dunia kama mgombea wao wa Urais Zanzibar  Othman Masoud Othman  ana ubavu  wa kumshinda  Rais Dk  Mwinyi. 

Hata hivyo Mbeto  aliendelea kumkanya Jussa huku akimtaka kuacha Siasa za jazba, uheke na udalali ,badala yake awe  mtu muungwana kwani kuna maisha mengine baada ya  uchaguzi na Siasa

"Huyu Ian Simiti wa Zanzibar  hajui maana ya  Siasa yeye muda wote anahemkwa na  chuki, gere na wivu wa jikoni . Aachana na Siasa za Miaka ya 1950 wakati Zanzibar ikipigania uhuru   .Siasa za ubaguzi na uhasama hazitakiwi tena  Zanzibar na kizazi kipya" Alisiaitiza

Katibu  huyo Mwenezi  alimueleza kinaganaga Jussa kuwa ameshiriki kuwafanya mizengwe  ili kuwazuia kina  Juma Duni Haji na Mohamed Dedes wasigombea urais huku akimpigia  debe Othman ili  kulinda maslahi  yake binafsi.

Post a Comment

0 Comments