Na mwandishi wetu
Mgombea ubunge kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Bi. Dorcas Francis Mwilafi, ameonesha dhamira ya kuleta mabadiliko katika Jimbo la Kawe baada ya kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo leo tarehe 15 Agosti 2025. Hatua hiyo imefanyika katika ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) ambapo alipokelewa na viongozi wa chama hicho pamoja na wafuasi wake.
0 Comments