NHIF, Mawakala wa Bima Wazindua Mpango wa Ushirikiano Kusajili Wanachama

 


Na mwandishi wetu

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa pamoja na Chama cha Mawakala wa bima nchini (IAAT) leo tarehe 13 Agosti, 2025 wamezindua mpango wa ushirikiano kwenye eneo la usajili wa wanachama, ikiwa ni mkakati mahsusi katika utekelezaji wa sheria ya bima ya afya kwa wote. 

Akizungumza katika uzinduzi wa mpango huo Mkurugenzi Mkuu wa NHIF Dkt. Irene C. Isaka amesema utekelezaji wa sheria ya bima ya afya kwa wote umeanza rasmi mwezi Agosti, 2024 baada ya kupitishwa kwa sheria ya bima ya afya kwa wote pamoja na kanuni zake na kutangazwa katika gazeti la serikali.

Dkt. Irene amesema utekelezaji wa sheria ya bima ya afya kwa wote, umeanza na wananchi mmoja mmoja au kipitia makundi mbalimbali wanaweza kujiunga na kunufaika na huduma za afya kupitia NHIF.

Dkt. Isaka aliendelea kusema,  Mfuko umewekeza katika Mifumo ya TEHAMA ili kurahisisha taratibu za usajili wa wanachama na huduma za Mfuko bila ya kikwazo cha kufika katika ofisi za Bima ya afya.

Dkt.Irene alisema asilimia 87 ya watanzania wote wapo katika sekta isiyo rasmi huku asilimia 13 tu, ndio wapo katika sekta rasmi, ni wakati sasa wa kuwafikia katika maeneo yao kuwasajili na huduma za bima ya afya na kuwahakikishia uhakika wa matibabu wakati wote.

Pia amewakumbusha Mawakala hao kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu ili kulinda taarifa za wanachama. Lakini pia aliwaadi ushirikiano katika kila hatua ikiwemo kila Meneja wa Mkoa kufanya mafunzo ya huduma za Mfuko ili Mawakala hao waweze kwenda kutoa elimu hiyo kwa wananchi kabla ya kuwasajili na huduma za NHIF. 

Hata hivyo Dkt. Isaka aliwajulisha Mawakala hao kuwa wanatakiwa kuwafikia wananchi na sio wananchi kuwafuata katika ofisi zao, vilevile mtizamo uwe kwenda kuuza vifurushi na sio kuuza magonjwa.

“tunakwenda kuuza vifurushi na sio magonjwa mwanachama aelezwe kwa undani kuhusu kifurushi na huduma ili kuweza kujiunga kwa wingi na kadiri tutakavyosajili wananchi wengi ndio watakasaidia wale wachache wanaougua kupata matibabu ya uhakika bila kikwazo cha fefha.

@wizara_afyatz @msemajimkuuwaserikali @bima_afyatz 

#nhiftz #bimayaafyakwawote #uhakikawamatibabukwa




Post a Comment

0 Comments